UFAHAMU JUU YA MVURUGIKO WA HOMONI KWA MWANAMKE


Mvurugiko wa homoni za mwanamke ni kitendo cha kuongezeka au kupungua kwa vichochezi katika mwili wa mwanamke pale anapo pata hedhi, hivyo kufanya mwili kubadilika. Mvurugiko huo huathiri kila mwanamke kwa zaidi ya 80%. Asilimia  kubwa ya wanawake mabadiliko huanza kati ya miaka 40 na 50, lakini pia kukosekana  kwa usawa wa homoni huweza kuonekana mapema zaidi, kuanzia miaka 14. Mabadiliko haya asilia hutokea wakati wa balehe, hedhi, ujauzito, kabla na baada ya ukomo wa hedhi. Mvurugiko wa homoni kwa mwanamke huweza kuchangiwa kutokuwepo na usawa katika homoni zifuatazo Estrogen, Progesterone na Testosterone. Kupungua au kuzidi kwa homoni hizi hupelekea mvurugiko  wa homoni kwa mwanamke.


                                                               II.        VYANZO VYA MVURUGIKO WA HOMONI


      Mvurugiko wa homoni ni tatizo linalowakumba wanawake wengi kwa sasa, hii ni kutokana na maisha wanayoishi, elimu finyu waliyonayo juu ya afya zao na kutokula kulingana na makundi ya damu. Vyanzo vya kuvurugika kwa homoni ni:

  • Uwepo wa sumu mwilini
  • Unbalanced Lifestyle (mfumo mbovu wa maisha)
  • Umri ukienda sana
  • Kukoma kwa hedhi
  • Kutofanya mazoezi
  • Uzito mkubwa
  • Mabadiliko ya mazingira au hali ya hewa
  • Msongo wa mawazo
  • Kula vyakula visivyo endana na Blood Group
  • Upungufu wa lishe mwilini
  • Matumizi ya  njia za kisasa za uzazi wa mpango
  • Utoaji wa mimba
  • Family History (Upungufu au ongezeko ya homoni ya progesterone na Estrogen)
  • Ongezeko la homoni ya Androgen (Kuota ndevu, sauti kama mwanaume)
  • Sababu za kibara (Ethnicity): Wanawake wa Afrika wengi wana hili tatizo la ongezeko ya Homoni ya Estrogen, ndiyo maana wana maumbile makubwa




  1. DALILI ZA MVURUGIKO WA HOMONI

Mfumo wa homoni ni muhimu sana kwa afya ya ubongo na miili yetu. Husaidia kuzuia magonjwa yasiyo ambukizi kadri umri unavyosonga mbele. Baadhi ya dalili zinazoweza kuonekana kwa mtu mwenye changamoto ya mvurugiko wa homoni ni kama vile:

-       Ukavu ukeni
-       Maumivu wakati wa tendo la ndoa
-       Kutoa jasho usiku
-       Maumivu chini ya kitovu wakati wa hedhi
-       Upungufu wa hamu ya tendo la ndoa
-    Mabadiliko ya siku za hedhi na kupata hedhi kwa muda mrefu unaozidi siku 7. (heavy bleeding, au kujaza pedi moja kwa saa moja)
-     Kukosa hedhi kwa muda mrefu, na kutoa damu yenye mabonge mabonge wakati wa hedhi
-       Uchovu wa mara kwa mara
-       Hasira za mara kwa mara
-       Kukosa usingizi
-       Homa za usiku na Kizunguzungu cha mara kwa mara
-       Mzio wa vyakula (Allergie), kuchaguachagua vyakula
-       Ongezeko ya tumbo na nyama uzembe
-       Kuharibika kwa ngozi (chunusi, vipele… n.k)
-       Maumivu ya viungo
-       Upungufu wa nywele  kichwani.
-       Kusahau sana (kukosa kumbukumbu)
-       Kuwa na hamu ya kula vyakula au vinywaji vya viwandani.
-       Kupata hedhi wakati wa ujauzito (progesterone ikiwa imezidi)
-       Kutokupata hedhi (balehe) adi umri wa miaka 20 na kuendelea
-       Mwili kutokukua, kuonekana kama binti mdogo, na kutokukua kwa via vya uzazi
-       Msongo wa mawazo na kukosa kujiamini
-       Kusinyaa na kupauka kwa
    ngozi wakati wa siku za hedhi na wakati wa utumiaji wa njia za uzazi wa mpango 
-       Maumivu ya kichwa mara kwa mara
-       Kuwa na tabia ya hamaki (kukosa utulivu)
-       Kutokupata choo kwa wakati
-       Misuli hudondoka





  1. MADHARA YA MVURUGIKO WA HOMONI
Pamoja na dalili nyingi tulizoziona tungependa wanawake waelewe vitu vifuatavyo hutokea iwapo atatumia njia za kisasa za uzazi wa mpango. Njia hizo husababisha saratani ya kizazi, CD4 kushuka, sehemu ya uke kuwa baridi, huchangia kwa 50% kufanyiwa upasuwaji (operation) wakati wa kujifungua, huathiri mtoto atakayezaliwa, huathiri ubongo (inapunguza uwezo wa kufikiria), kutokwa na majimaji yenye harufu mbaya ukeni na magonjwa ya mara kwa mara.

Ukiendelea kubaki na dalili tajwa hapo awali kwa muda mrefu, kinga ya mwili itashuka kwa kiasi kikubwa na kusababisha madhara mengi kama yafuatayo:

  • Kutoshika ujauzito kwa muda mrefu
  • Mimba kuharibika mara kwa mara
  • Kukosa mtoto au Ugumba
  • Maumivu wakati wa tendo la ndoa
  • Kuwa na tabia na maumbile ya kiume
  • UTI (Urinary Tract Infection)
  • Kuzeeka mapema
  • Kuziba kwa mirija ya uzazi
  • Uvimbe (Fibroids and Cysts)




  1. SULUHISHO

  1. Suluhisho Linalopendwa
Wanawake wengi baada ya kujifahamu kuwa homoni zao haziko sawa huenda mahospitalini ambako hupewa madawa (bioidentical or synthetic hormones) na wengine hufanyiwa hormone replacement therapy.
Tiba hii huandaliwa kwa ajili ya kuzifanya homoni zifanye kazi zake kama kawaida. Lakini hupelekea madhara kama:
-       Kuongeza uwezekano wa shinikizo la damu.
-       Osteoporosis.
-       Madhara katika mfumo wa uzazi.
-       Saratani na mengineyo.


  1. Suluhisho La kudumu

Mvurugiko wa homoni unasababishwa na upungufu wa lishe, msongo wa mawazo, na uwepo wa sumu mwilini na hivi vyote ni vitu unavyoweza kurekebishika. Kwa wanawake wenye changamoto hii tumewaandalia  program ya lishe kamili na virutubisho muhimu. Program hii ni ya vyakula; sio dawa wala miti shamba. Inasaidia kuweka sawa homoni za mwanamke, kuboresha mfumo mzima wa uzazi, kuleta heshima ya ndoa maana uke utarudi katika hali yake ya asili (mnato na ute ute ukeni wenye kuleta msisimko wakati wa tendo la ndoa, na kupunguza kasi ya uzee). Sumu zikizidi mwilini mwanamke huzeeka kabla ya wakati na kupatwa na changamoto mbalimbali za kiafya ikiwemo: vimbe zinazo jipachika kwenye uzazi wa mwanamke, vidonda vya tumbo, … n.k.
Kwa yeyote anayehitaji hii program ya kuboresha na kuimarisha Afya yake awasiliane na kampuni kwa namba zifuatazo


                                                     +255 717 795 966 










Comments

Popular posts from this blog

UFAHAMU WA KINA KUHUSU TATIZO LA BAWASIRI.

FAHAMU AFYA YA TEZI DUME - PROSTATE GLAND